Mfumo wa Utawala
Jiografia, Habari ya Idadi ya Watu
Mila, Tamaduni

Sera za uhamiaji

Afya, Kazi, Elimu

Huduma, Taasisi, Ushauri
Uko hapa:  Sera za uhamiaji / Haki za kimsingi na majukumu ya wananchi wa mataifa ya tatu

Haki za kimsingi na majukumu ya wananchi wa mataifa ya tatu

Βασικά Δικαιώματα και Υποχρεώσεις πολιτών τρίτων χωρών


Usafiri

Naweza kusafiri kotekote nchini Ugiriki?

Ndio! Iwapo wewe ni raia wa mataifa ya tatu na unaishi nchini na stakabadhi hitajika, uko huru kusafiri na kuishi popote utakapo nchini.


Afya

Nina haki ya kuchukua bima?

Ndio! Iwapo wewe ni raia wa mataifa ya tatu na unaishi nchini na stakabadhi hitajika, unaweza kuchukua bima (kulingana na hali yako ya kitaaluma) katika mashirika faafu ya bima. Una haki sawa za bima kama raia wa Ugiriki.

Je, lazima nitoe malipo ili kupata matibabu na huduma za hospitali?

Hapana! Iwapo wewe ni raia wa mataifa ya tatu na unaishi nchini na stakabadhi hitajika, una haki ya kupata matibabu ya bure katika mashirika ya umma ya Mfumo wa Afya wa Kitaifa (ESY), kama raia wa Ugiriki. Utapata habari zaidi katika sura ya afya.

Je, nikiingia katika taasisi, naweza kupata maelezo kwa lugha nitakayoelewa?

Ndio! Ukiingia katika taasisi, una haki ya kujulishwa sheria zake, sawia na haki na wajibu wako. Mawasiliano yako yafaa kuelekezwa na mwanadiplomasia au maafisa wa ubalozi wa nchi, na ambayo wewe ni raia au ulitoka, pamoja na mawakili wako.


Elimu

Iwapo sijahitimu miaka 18, ni lazima niwe shuleni?

Iwapo unaishi Ugiriki umejumuishwa katika masomo ya lazima, kama raia wa Ugiriki. Watoto wa chini wa miaka 18, wanaoshiriki viwango vyote vya elimu, wana uhuru wa kushiriki shughuli zote shuleni au katika jumuiya ya elimu. Haki ya elimu kwa watoto wa kigeni walio chini ya miaka 18 haina mjadala.(Imehakikishwa na Mkataba wa Kimataifa kuhusu Haki za Mtoto (Ibara ya 28) na sheria ya Kigiriki katika Katiba ya Ugiriki (Ibara 16 & 21) na katika nyaraka mbalimbali kama 73025/C2/2010. Habari zaidi ni katika sura ya Elimu).

Ni nini kinachohitajika ili kumsajilisha mtoto wa chini ya miaka 18 (kutoka nchi ya kigeni) katika shule za Ugiriki za ngazi zote?

Ili kumsajili mtoto wa chini ya miaka 18 katika shule za Kigiriki katika ngazi zote, stakabadhi muhimu zinazotolewa kwa raia wa Ugiriki zinahitajika.

Hata hivyo! Watoto (raia wa nchi za tatu) wanaweza kujiunga na shule za umma iwapo hawana stakabadhi za kutosha, iwapo: a) Wanalindwa na Serikali ya Ugiriki chini ya ulinzi wa kimataifa, na walio chini ya ulinzi wa Ubalozi wa Umoja wa Mataifa, b) Wametoka maeneo ambayo hali si tulivu, c) Wametuma ombi la ulinzi wa kimataifa d) Ni raia wa mataifa ya 3 wanaoishi Ugiriki, hata iwe uhalali wa makazi yao bado hujathibitishwa. (Habari zaidi katika sura ya Elimu).

Je, ninaweza kupata elimu ya juu/Chuo Kikuu?

Ndio!Ikiwa una elimu ya sekondari nchini Ugiriki nawe ni raia wa mataifa ya tatu, unaweza kupata elimu ya juu chini ya masharti yale yale ya raia wa Ugiriki (kwa mujibu wa masharti ya sheria iliyoko).


Dola

Je, wajibu wangu ni nini kwa huduma za utawala wa Mashinani nchini, au kwa wakurugenzi wa sera za uhamiaji katika Wizara ya Mambo ya ndani?

Katika kukaa kwako nchini Ugiriki, lazima ufahamishe mamlaka ya Utawala wa Mashinani nchini, au Wakurugenzi wa Sera za Uhamaji katika Wizara ya Mambo ya Ndani:

    a) Mabadiliko yoyote ya anwani yako ya makazi,
    b) mabadiliko yoyote ya hali yako binafsi, hasa mabadiliko ya uraia, utambuzi, kuvunjwa kwa ndoa au kujifungua
    c) Kupoteza au kufanya upya vipengele vya pasi yako ya kusafiria au stakabadhi nyingine za kusafiri
    d) kupotea kwa kibali cha makazi au Kijitabu chamakazi au makazi ya kudumu

Je, ni wakati gani italazimu niondoke nchini?

Kwa masikitiko, iwapo una kibali cha makazi, lazima uondoke bila taarifa zaidi, kabla ya siku ya mwisho ya kumalizika kwa kibali chako, isipokuwa tu kama kabla ya kumalizika kwa muda huo uwe umetuma ombi la kufanya upya, na uwe umepata kibali cha aya ya 7 ya Ibara ya 8 na aya ya 5 ya ibara ya 9 ya Kanuni za Uhamaji L.4251/2014.

Kumbuka: Unaweza kupata orodha ya mashirika yanayotoa msaada wa kisheria katika sura ya mwisho.

Rudi
Mradi wa 1.4.b/13 ‘Matangazo ya Redio ya masuala kuhusiana na wahamiaji, uzazi, na usambazaji mpana wa vifaa vilivyochapishwa, vya sauti na vielelezo’ ulifadhiliwa 95% na Hazina ya Jumuiya na 5% na Rasilimali za Kitaifa