Mfumo wa Utawala
Jiografia, Habari ya Idadi ya Watu
Mila, Tamaduni

Sera za uhamiaji

Afya, Kazi, Elimu

Huduma, Taasisi, Ushauri
Uko hapa:  Huduma, Taasisi, Ushauri / Usafiri

nawezaje kufikia maeneo mbalimbali ya Ugiriki?

metro

Kutokana na upekee wa upeo wa ardhi ya Ugiriki na visiwa vyake vingi, malengo yameeelekezwa sio tu kwa uchukuzi wa barabarani, bali pia kwa usafiri wa majini.

Usafiri wa masafa marefu.

Usafiri wa masafa marefu nchini Ugiriki hutolewa na:

Treniusafiri:

    Kampuni hii sasa ni huru kutoka KIKUNDI CHA OSE (Shirika la Reli la Heleniki). Ndiyo kampuni tu inayotoa usafiri wa treni nchini Ugiriki. TRAINOSE huunganisha mikoa, masafa marefu, na vitongoji.
Mabasi ya masafa marefu:
    Kampuni ya KTEL ndiyo kampuni inayotoa usafiri wa kuunganisha miji nchini Ugiriki kwa kutumia mabasi. Jina KTEL hutumika pia kurejelea stesheni za kuabiria mabasi. KTEL pia ina ukiritimba katika utoaji wa huduma za usafiri.
Uchukuzi wa angani:
    Nchi ya Ugiriki ina viwanja kadhaa vya kimataifa na kitaifa vya ndege, ambapo mashirika mbalimbali ya ndege hupatikana na hutoa huduma za uchukuzi wa angani na kuunganisha miji mikuu ya mikoa, na pia Atheni na visiwani. Aidha, hutoa uchukuzi wa kimataifa na kuunganisha miji kadhaa ya Ugiriki na viwanja vikubwa vya ndege vya Ulaya.

Usafiri wa majini na bandarini

Nchini Ugiriki kuna usafiri wa majini unaounganisha bandari kubwa za bara na visiwa, ukiwahudumia maelfu ya wenyeji na watalii, hususan wakati wa majira ya joto.

    oKuondoka/kuwasili kwa mashua Tel. 14944
    Bandari ya Piraeusi Tel. 2104226000, (www.olp.gr)
    Bandari ya Rafina Tel. 2294022300, 2294022481
    Bandari ya Lavurio Tel. 2292025249
    Bandari ya Agiosi Konstantinosi Tel. 2235031759

Visiwa vikubwa vimeunganishwa na bandari zilizotajwa hapo juu na huduma za mara kwa mara kwa mwaka mzima. Hata hivyo, kuna upungufu na kuvunjwa kwa njia za kwenda na kutoka baadhi ya visiwa wakati wa baridi. Visiwa hivi huitwa laini iso faida, na kwa kawaida huwa vidogo na vyenye wakazi wachache. Jina la eneo hili la laini hutokana na ukweli kwamba uhusiano wowote na kisiwa hiki, uwe ni kwa njia ya feri au ndege, huruzukiwa na serikali. Visiwa laini viso faida ni vingi, kama vile Irakleia, Anafi, Kasterlorizo, na Asitipalaia.

Usafiri wa mijini na miji ya Ugiriki

Atheni

Mfumo wa uchukuzi wa umma wa Atheni hujumuisha mfumo wa chini ya ardhiwa reli (Metro), tramu, mabasi na troli, huku sehemu ya huduma za usafiri zikishughulikiwa na Reli ya Vitongoji vya Jiji. Katika sehemu zingine za Atika, huduma nyingi zaidi za uchukuzi hutolewa na kampuni ya KTEL iunganishayo miji, na sehemu ilosalia ikisimamiwa na reli ya vitongoji na mabasi ya mjini.


    Treni za kizazi cha kwanza– AtheniMetro
    Treni za kizazi cha pili - Atheni Metro
    Treni ya kizazi cha tatu – AthensMetro Picha
    Kituo cha Chalandri, AtheniMetro (Line 3)

Shirika la Uchukuzi wa Mjini la Atheni (OASA) husimamia sehemu kubwa ya wilaya, huku matawi yake, Uchukuzi wa Barabarani SA (OSY) na Uchukuzi wa Reli Mjini SA (STASY) husimamia utekelezaji wa usafiri, na kuna ushirikiano na TRAINOSE SA, kutokana na kuwepo kwa sehemu ya tovuti wake (Reli ya Vitongoji) ndani ya mfumo wa miji ya Atheni. Kwa wilaya nyinginezo, usimamizi wa usafiri umekabidhiwa Mamlaka ya Udhibiti wa Usafri wa Abiria, na utekelezaji wake hufanywa na KTEL Atika SA.


    Treni ya Reli ya Vitongoji, Atheni
    Basi katika Mraba wa Omonoia
    Basi Troli katika barabara ya Patisioni
    Treni ya Tramu katika Irinisi na Kituo cha Uga wa Filiasi
    Treni ya Tramu katika mraba wa Sintagima
    Basi Troli katikati mwa Jiji la Atheni

Kwa habari zaidi zinazohusiana na ratiba za uchukuzi wa umma, angalia vituo maalum vya simu na tovuti zao:

  • Ratiba ya mabasi ya jijini: tel. 185, www.oasa.gr
  • Atiko Metro: tel. 210 5194001, www.ametro.gr
  • Reli ya vitongoji: tel. 210 5272000, www.proastiakos.gr
  • Atheni Tramu: tel. 210 9978000, www.tramsa.gr
  • Reli ya Mjini ya umeme: tel. 210 3248311, 1440, www.isap.gr
  • Shirika la Reli la Heleniki: tel. 210 5297777, www.ose.gr
  • Vituo vya Mabasi vya unganiko la miji: tel. 1440, 210 5124910, www.ktel.org
  • o Basi la Umma la kujione Mandhari N.400: tel. 185

Thesaloniki

Katika Thesaloniki, utoaji wa huduma za usafiri husimamiwa na Shirika la Huduma za Usafiri la Thesaloniki) ambalo huunganisha mji huo na makazi ya wengi mkoani. Reli ya vitongoji vya Thesaloniki huunganisha mji na makazi ya wengi mkoani, na miji iliyo nje ya wilaya kama vile Larisa, Katerini, Veroia and Edesa.

Patra

Katika Patra, usafiri wa mjini husimamiwa na KTEL. Vitongoji vya Patra hutumia treni za miji (Proastiakos), ambazo ziko chini ya usimamizi wa TRAINOSE, zikiunganisha Patra na Rio pamoja na vitongoji vinginevyo vya jiji.


Rudi
Mradi wa 1.4.b/13 ‘Matangazo ya Redio ya masuala kuhusiana na wahamiaji, uzazi, na usambazaji mpana wa vifaa vilivyochapishwa, vya sauti na vielelezo’ ulifadhiliwa 95% na Hazina ya Jumuiya na 5% na Rasilimali za Kitaifa