Mfumo wa Utawala
Jiografia, Habari ya Idadi ya Watu
Mila, Tamaduni

Sera za uhamiaji

Afya, Kazi, Elimu

Huduma, Taasisi, Ushauri
Uko hapa:  Mfumo wa Utawala / Mfumo wa Kisiasa / Mamlaka ya Kisheria

Mamlaka ya Kisheria

Legislative powerWanachama wa Bunge la Kigiriki huchaguliwa na wananchi waliohitimu umri wa miaka 18. Ina wajumbe 300, waliochaguliwa kwa muhula wa miaka mine, na mfumo wa kushinikiza uwakilishi sawai katika maeneo ya uwakilishi Bungeni 48 ya viti vingi, maeneo 8 ya kiti kimoja, na orodha moja ya kitaifa. Wabunge 288 juu ya 300 huchaguliwa moja kwa moja na wananchi, kwani wananchi wanaweza kutangaza wanayempendelea kwa kuchagua majina yao kwenye debe. Viti 12 vilivyosalia huchaguliwa na orodha za kitaifa za vyama, kwa msingi wa ukubwa wa vyama na uwiano wa jumla ya kura za kila chama katika uchaguzi. .

Sheria hii ya uchaguzi imeweka mfumo tata wa kushinikiza uwakilishi sawia ambao hupendelei kuundwa kwa vyama vidogo, na huwezesha wingi wa walio wengi Bungeni japo hana wingi mkubwa wa watu. Kila chama lazima kiwe na walau 3% ya kura ili kuchagua wanachama Bungeni. Chama tawala chaweza kupata wingi wa watu bungeni (walau wabunge 151), almuradi kipate walau 41% ya kura za umaarufu. Sheria ya uchaguzi inaweza kubadilishwa kwa wingi kidogo wa Wabunge, lakini sheria hiyo mpya haiwezi kutumika kwa uchaguzi unaofuatia, bali chaguzi za baadaye, ila tu ipigiwe kura na idadi kubwa – 2/3 ya jumla ya idadi ya Wabunge.

Legislative power

Rudi
Mradi wa 1.4.b/13 ‘Matangazo ya Redio ya masuala kuhusiana na wahamiaji, uzazi, na usambazaji mpana wa vifaa vilivyochapishwa, vya sauti na vielelezo’ ulifadhiliwa 95% na Hazina ya Jumuiya na 5% na Rasilimali za Kitaifa