Mfumo wa Utawala
Jiografia, Habari ya Idadi ya Watu
Mila, Tamaduni

Sera za uhamiaji

Afya, Kazi, Elimu

Huduma, Taasisi, Ushauri
Uko hapa:  Jiografia – Habari ya Idadi ya Watu / Jiografia / Visiwa

Visiwa

Ugiriki ina visiwa takribani 2,500. Kati ya visiwa hivi, ni 165 ambavyo watu wanaishi:


Visiwa vingi vinapatikana Eejeni, na vimegawanyika katika sehemu saba (kutoka kaskazini hadi kusini):

  • Visiwa vya kaskazini mashariki mwa Eejeni: Agiosi, Efustratiosi, Thasosi Ikaria, Lesibosi, Limnosi, Oinousesi, Samosi, Samothuresi, Chiosi, Pusara
  • Siporadesi: Alonisosi, Skiathosi, Sikopelos, Skairosi
  • Yuboea
  • Visiwa vya Saronika: Ajistiri, Eejina, Methana, Porosi, Salamina, Sipetisesi, Haidura
  • Saikiladesi: Safu ya visiwa 56, hususan Amorigosi, Anafi, Andurosi, Antiparosi, Delosi, Iosi, Tizia (Kea), Kimolosi, Kithinosi, Milosi, Mikonosi, Nakusosi, Parosi, Santorini, Serifosi, Sikinosi, Sifunosi, Sirosi, Tinosi, Folegandurosi, na zile saikaledi ndogo zinazojumuisha • Donousa, Irakileia, Koufonisia, na Sikoinousa.
  • Dodekanesi: Asitipalaia, Kalimunosi, Karipathosu, Kasosu, Kasutelorizo, Kosu, Leipusoi, Lerosi, Nisirosi, Patimosi, Rodesi, Simi, Tilosi, Chalaki
  • Krete

Bahari ya Loniani huwa na safu moja tu ya visiwa:

    Visiwa vya Loniani: Zante, Ithaki, Korfu, Kefalonia, Lefukada, Pasoi na Kithira, ambavyo vinapatikana mkabala na Peloponesi, ndivyo vikubwa zaidi kati ya visiwa vya Loniani, na huunda Epitanesi. Visiwa vingine vy Loniani ni pamoja na: Antipakisoi, Antikithira, Ereikousa, Kalamosi, Kasitosi, Mathiraki, Meganisi, Othonoi, Sikoripiosi, Sitirofadesi.

Visiwa ambavyo si sehemu ya safu yoyote ya visiwa, lakini vyenye fahari ya uzuri wa asili, ni pamoja na visiwa vya Gavudosi (Kusini mwa Krete), Elafonisosi (katika Ghuba ya Lakoniki), na Trizonia (katika Ghuba ya Korintho).

Baadhi ya ustaarabu kongwe zaidi za Ulaya zimeendelezwa katika visiwa vya Ugiriki (Sikiladiki, Minoiki, nk.). Visiwa hivi vina maeneo ya kipekee ya akiolojia, na urithi wa mila haiba za utamaduni maridhawa wa kudumu.


Rudi
Mradi wa 1.4.b/13 ‘Matangazo ya Redio ya masuala kuhusiana na wahamiaji, uzazi, na usambazaji mpana wa vifaa vilivyochapishwa, vya sauti na vielelezo’ ulifadhiliwa 95% na Hazina ya Jumuiya na 5% na Rasilimali za Kitaifa